BONYEZA HAPA CHINI KUSIKILIZA LIVE

Friday, June 10, 2016

KARAGWE YAFUNGUA FURSA ZA AJIRA KWA WANAWAKE NA VIJANA KWA KUTOA MIZINGA YA KUFUGA NYUKI 1000 YENYE THAMANI YA MILIONI 70


Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe yatengeneza nafasi za ajira kwa wananwake na vijana kwa kutengeneza mizinga ya nyuki 1000 na kuigawa kama mikopo kwa vikundi arobaini vya vijana na wanawake kwa ajili ya kuzalisha asali na  kujiajili ili kupunguza tatizo la ajira katika wilaya hiyo.

Mizinga 1000 ambayo tayari imetengenezwa yenye thamani ya shilingi milioni 70 iligawiwa kwa vikundi 40 vya vijana na akina mama kila kikundi mizinga 25 na zoezi hilo la ugawaji wa mizinga hiyo lilizinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu Juni 8, 2016 katika Halmashauri hiyo.

Akitoa taarifa ya utengenezaji wa mizinga hiyo Kaimu Mkuregenzi Mtendaji  wa Halmashauri hiyo Bi. Ashura Kajuna (Afisa Uchaguzi) alisema kila kikundi kitakopeshwa mizinga 25 na vikundi hivyo 40 vitapewa kipindi cha neema (Grace Period) ya miezi 12 aidha mikopo hiyo ya mizinga itarejeshwa ndani ya muda miezi 24 kwa kuzingatia ufaugaji wa nyuki.

Aidha, Bi Ashura alisema ili kikundi kikidhi vigezo vya kupatiwa mkopo wa mizinga hiyo lazima kiwe kimesajiliwa na Halmashauri na taasisi nyingine za Serikali, kikundi lazima kiwe cha wanawake au vijana pia kiwe na uzoefu wa ufugaji wa nyuki na maeneo ya kufugia yenye malisho yenye malisho ya kutosha (Bee fodders)

Mkuu wa Mkoa Mhe. Kijuu aliishukuru Halmashauri ya Wilaya Karagwe kwa kutengeneza mizinga 1000 na kuwaasa vijana kuchangamkia fursa hiyo ya ajira ili wajiingizie kipato kwa kufuga nyuki na kuzalisha mazao yake kama asali ambayo alisema ina soko kubwa ulimwenguni pote. Pia alisema kuwa huo ni mradi mzuri hasa kwa kutunza mazingira kwani  nyuki wakifugwa miti haitakatwa hovyo hovyo.

Mama Victoria Clemence ni mwanakikundi wa kikundi cha Wanambingu cha Kayanga ambaye alipokea mizinga 25 kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wakati wa uzinduzi kwaniaba ya wanakikundi wenzake alisema kikundi chao tayari wameanza kunufaika na ufugaji wa nyuki kwani tayari wameanza kuuza asali na kujiingizia kipato, aidha, mizinga hiyo 25 itaongeza uzalisha wa asali na kukuza kipato cha kikundi chao.

Katika hatua nyingine Kampuni ya National Beekeeping Supplies Ltd iliyopewa tenda ya kutengeneza mizinga 1000 na Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe kupitia kwa Mkurugenzi  wake mkuu  Bw. Kaizilege Daudi ilitoa vifaa vya kulina asali vyenye thamani ya shilingi 2,125,000/= ili kuvisaidia vikundi vilivyokopeshwa mizinga kulina asali yenye ubora.

Vikundi vilivyogawawi mizinga ya mkopo vinatemea kunufaika kwa  uzalishaji wa asali kwa wastani  wa kila mzinga kwa msimu ( mwaka mmoja) kuzalisha lita 10 za asali na kikundi  kimoja kinapatiwa mizinga 25, ambapo wastani wa bei ya asali kwa lita moja ni shilingi 8,000/= (10x25x8,000/= = 2,000,000/=) Kwahiyo kila kikundi kimoja kila mwaka kitakuwa kinaingiza shilingi 2,000,000/= kwa kila mwaka.


 
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu 

No comments:

Post a Comment